Jua kidogo hichi kuhusu saratani kutoka kwa WHO

Shirika la afya duniani WHO linasema saratani ndio chanzo cha kifo cha mtu mmoja kati ya sita duniani,Idadi ya visa vipya vya ugonjwa huo vinatarajiwa kuongezeka kwa takriban asilimia sabini katika miongo miwili ijayo.
 Tokeo la picha la saratani


*Mambo kumi unayoweza kufanya kupunguza hatari ya kuugua saratani*:
 -Usivute sigara wala kutumia tumbaku ya aina yoyote -
-Hakikisha nyumbani kwako hamna moshi
-Kula chakula chenye afya
 -Kunyonyesha kunapunguza hatari kwa mama kuugua saratani
 -Hakikisha watoto wako wanapata chanjo dhidi ya hepatatis B na HPV
 -Epuka kuchomwa sana na miale ya jua, au tumia mafuta yanayo kukinga dhidi ya miale hiyo. -Punguza uchafuzi wa hewa ndani na nje ya nyumba -Jishughulishe kuupa mwili mazoezi -Punguza unywaji wa pombe -Jitahidi kufanyiwa ukaguzi wa mapema kutambua uwepo wa saratani

No comments